Mkemia Mkuu wa Serikali Zanzibar, Dkt. Farid Mpatani (kushoto), akiuliza swali kwa Mtaalam wa Maabara, Everlight Matinga (katikati) kuhusu uchunguzi wa maikrobaiolojia mara baada ya kutembelea maabara ya Maikrobaiolojia wakati wa ziara ya kikazi ya kubadilishana uzoefu na kuimarisha uhusiano wa kiutendaji waliyofanya Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali, Dar es Salaam
-
-
Mkemia Mkuu wa Serikali ya Zanzibar, Dkt. Farid Mpatani, (kulia), akimsikiliza Meneja wa Maabara ya Sayansi Jinai Kemia, Fidelis Segumba (kushoto) kuhusu namna uchunguzi wa kimaabara wa dawa za kulevya unavyofanyika katika maabara hiyo wakati wa ziara yake ya kikazi aliyofanya Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali Bara.
-
Mkemia Mkuu wa Serikali Zanzibar, Dkt. Farid Mpatani (kushoto), akipata ufafanuzi kuhusu uchunguzi wa sampuli mbalimbali za mazingira unavyofanyika kwenye Maabara ya Mazingira kutoka kwa Mtaalam wa Maabara, Alois Ngonyani (kulia) wakati wa ziara ya kikazi aliyofanya Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali Bara.
-
Mkemia Mkuu wa Serikali Zanzibar, Dkt. Farid Mpatani (kushoto), akipata ufafanuzi kuhusu uchunguzi wa sampuli mbalimbali za mazingira unavyofanyika kwenye Maabara ya Mazingira kutoka kwa Mtaalam wa Maabara, Alois Ngonyani (kulia) wakati wa ziara ya kikazi aliyofanya Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali Bara.
-
Watumishi wa Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali, Dar es Salaam, wakiwa pamoja kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja katika kilele cha maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani kwa mwaka 2023.
-
Watumishi wa Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali, Dar es Salaam, wakiandamana na kupita mbele ya mgeni rasmi, Mhe. Amos Makala (hayupo pichani) wakati wa maadhimisho ya siku ya Wanawake Duniani Machi 8,2023, ambapo kwa Mkoa wa Dar es Salaam yalifanyika kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja.
-
Watumishi wa Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali, Dar es Salaam, wakiwa pamoja kabla ya kuelekea viwanja vya Mnazi Mmoja katika kilele cha maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani kwa mwaka 2023.
-
Washiriki wa mafunzo wakimsikiliza Mkemia Mkuu wa Serikali, Dkt. Fidelice Mafumiko (hayupo pichani) akiongea wakati wa kufunga mafunzo ya udhibiti wa Matukio ya sumu kwa Maafisa Afya ya Jamii ngazi ya Kata na Mitaa kutoka Wilaya ya Ilala.
-
Mkemia Mkuu wa Serikali, Dkt. Fidelice Mafumiko (aliyesimama) akiongea wakati wa kufunga mafunzo ya uelewa kuhusu kudhibiti matukio ya sumu kwa Maafisa Afya wa Kata na Wahudumu wa Afya ya Jamii ngazi ya Mitaa. Mafunzo hayo yalifanyika katika makundi mawili, Kundi la kwanza Februari 20, 2023, na kundi la pili Februari 21, 2023 katika Ukumbi wa Tume ya Ushindani, Jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mwakilishi Ofisi ya Mganga Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Anence Kamasho, na kushoto ni Mratibu wa Kituo cha Taifa cha Kudhibiti Matukio ya Sumu, Yohana Goshashy.
-
Mkemia Mkuu wa Serikali, Dkt. Fidelice Mafumiko (aliyesimama), akizungumza na watumishi wa Mamlaka (hawapo pichani), wakati akifungua mafunzo kuhusu Mkakati wa Mapambano dhidi ya Rushwa Mahala pa Kazi. Mafunzo hayo yamefanyika katika ofisi ndogo ya Mamlaka, jijini Dar es Salaam, Februari 17, 2023.
-
Katibu Msaidizi Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma, Dar es Salaam, Bi. Elizabeth Komba (aliyesimama), akiwasilisha mada kuhusu Mkakati wa Mapambano dhidi ya Rushwa Mahala pa Kazi kwa watumishi wa Mamlaka na kuwasisitiza watumishi kuhakikisha wanakuwa waadilifu katika kusimamia shughuli za Serikali.
-
Mkemia Mkuu wa Serikali, Dkt. Fidelice Mafumiko (aliyesimama), akiongea na wanafunzi wa kozi ya Kemia ya Petroli (Petroleum Chemistry), kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, kuhusu majukumu ya Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali (GCLA) katika ukumbi wa Mamlaka uliopo Ofisi ndogo ya Dar es Salaam, Februari 17, 2023. Lengo kuu ya ziara hiyo ni kufahamu namna GCLA, inavyotekeleza majukumu yake mbalimbali haswa katika shughuli za uchunguzi wa kimaabara. Jumla ya Wanafunzi 18 wamepata fursa ya kutembelea Maabara mbalimbali za Mamlaka.
-
Mkurugenzi wa Huduma za Sayansi Jinai, David Elias (aliyekaa katikati), akiwa na Watumishi wa Mamlaka, Meneja wa Maabara ya Maikrobaiolojia, Faustine Wanjala (wa pili kushoto, waliokaa), Kaimu Meneja wa Maabara ya Mazingira, Alois Ngonyani (aliyekaa kushoto) pamoja na wanafunzi wa kozi ya Kemia ya Petroli kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam waliotembelea maabara za Mamlaka kwa ajili ya kujifunza kwa vitendo.
-
Mtumishi wa Mamlaka, Alois Ngonyani (kulia), akiwaelezea wanafunzi wa kozi ya Kemia ya Petroli kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam namna uchunguzi unavyofanyika katika Maabara ya Mazingira.
-
Mtumishi wa Mamlaka, Glory Mushi (kulia), akiwaonyesha kwa vitendo wanafunzi namna uchunguzi wa kimaabara unavyofanyika katika mitando iliyopo katika Maabara ya Mazingira katika Ofisi ndogo ya Dar es Salaam
-
Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Pugu, wakisikiliza mada mbalimbali zilizokuwa zinawasilishwa na maafisa kutoka Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali (hawapo pichani), wakati walipotembelewa na GCLA, kwa lengo la kuwaelimisha kuhusu ya majukumu ya Mamlaka pamoja na matumizi salama ya kemikali.
-
Mtumishi wa Mamlaka, Everlight Matinga (aliyesimama kushoto), akitoa elimu kwa wanafunzi wa Shule ya Sekondari Pugu iliyopo jijini Dar es Salaam, kuhusu majukumu mbalimbali yanayotolewa na Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali (GCLA), yakiwemo Usimamizi wa Sheria ambazo lengo kuu ikiwa ni kulinda usalama wa watu na mazingira katika matumizi ya kemikali na Vinasaba vya Binadamu. Utoaji elimu hiyo umefanyika katika ukumbi wa Shule ya SekondarI Pugu, Februari 17, 2023.
-
Waziri wa Afya, Mhe. Ummy Mwalimu (aliyekaa katikati) Mwakilishi wa Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Daud Masasi (kulia kwa Waziri) Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka, Profesa Esther Lugwisha (kushoto kwa Waziri), Mkemia Mkuu wa Serikali, Dkt. Fidelice Mafumiko(kulia) pamoja na Mkurugenzi wa Tiba kutoka Wizara ya Afya, Profesa Paschal Ruggajo (kushoto) wakiwa pamoja na Wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka na Wakurugenzi wa Wizara ya Afya mara baada ya kukamilika kwa hafla ya kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa Jengo la Makao Makuu ya Mamlaka, jijini Dodoma iliyofanyika Februari 11, 2023
-
Waziri wa Afya, Mhe. Ummy Mwalimu (kulia) na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka, Profesa Esther Lugwisha (kushoto) wakifungua pazia kuashirikia uwekaji rasmi wa jiwe la msingi la jengo la Makao Makuu ya Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali jijini Dodoma Februari 11, 2023.
-
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka, Profesa Esther Lugwisha, akiongea wakati wa hafla ya kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa jengo la Makao Makuu ya Mamlaka iliyofanyika Februari 11, 2023 katika Ofisi za Mamlaka jijini Dodoma.
-
Waziri wa Afya, Mhe. Ummy Mwalimu (kulia) akitoa hotuba wakati wa hafla ya kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa jengo la Makao Makuu ya Mamlaka iliyofanyika Februari 11, 2023 katika Ofisi za Mamlaka zilizopo Barbara ya Mkemia Mkuu wa Serikali, Mtaa wa Secherela, Kata ya Tambukareli, Kitalu “AC” jijini Dodoma.
-
Waziri wa Afya, Mhe. Ummy Mwalimu (kulia) akimsikiliza Mtumishi wa Mamlaka, Leticia Waitara (kulia) wakati Mhe. Waziri wa Afya alipokuwa anatembelea maabara zilizopo katika jengo la Makao Makuu ya Mamlaka jijini Dodoma kabla ya kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa jengo hilo Februari 11, 2023.
-
Waziri wa Afya, Mhe. Ummy Mwalimu (wa pili kushoto) akiwa ameambatana na Wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka na Wakurugenzi kutoka Wizara ya Afya kwa ajili ya kutembelea maeneo ya jengo hilo kabla ya kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa jengo la Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali Dodoma Februari 11, 2023.
-
Waziri wa Afya, Mhe. Ummy Mwalimu (kushoto) akisamiliana na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka, Profesa Esther Lugwisha (katikati) baada ya Waziri kuwasili katika Jengo la Makao Makuu ya Mamlaka, jijini Dodoma kwa ajili ya hafla ya kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa jengo hilo Februari 11, 2023. Upande wa kulia ni Mkemia Mkuu wa Serikali, Dkt. Fidelice Mafumiko, akishuhudia.
-
Kaimu Meneja wa Maabara ya Sayansi Jinai Toksikolojia, Kagera Ng’weshemi (aliyevaa maski), akiwaonesha Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii picha zinazohusiana na mfano wa sampuli/vielelezo vinavyosadikiwa kuwa ni dawa za kulevya zilizowasilishwa maabara kwa ajili ya uchunguzi ili kuthibitisha endapo ni dawa za kulevya.
-
Kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii, Mhe. Aloyce John Kamamba, wa pili kutoka kulia ni Naibu Waziri wa Afya, Mhe. Dkt. Godwin Mollel, wakiwa na Mkemia Mkuu wa Serikali, Dkt. Fidelice Mafumiko (wa pili kutoka kushoto), akiwaongoza Waheshimiwa Wabunge hao ambao ni Wajumbe wa Kamati kuelekea katika Maabara ya Sayansi Jinai Baiolojia na Vinasaba.
-
Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii, wakifuatilia Taarifa ya Utekelezaji wa Majukumu ya Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali, iliyokuwa ikiwasilishwa na Mkemia Mkuu wa Serikali, Dkt. Fidelice Mafumiko (hayupo pichani).
-
Naibu Waziri wa Afya, Mhe. Dkt. Godwin Mollel (aliyesimama), akizungumza na Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii, walipotembelea Ofisi ndogo ya Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali (GCLA) iliyopo Dar es Salaam, Februari 4, 2023. Lengo kuu ya ziara hiyo ni kufahamu namna Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali inavyotekeleza majukumu yake haswa katika shughuli za uchunguzi wa kimaabara ambapo waliweza kutembelea maabara za Sayansi Jinai Toksikolojia, Sayansi Jinai Kemia, Sayansi Jinai Baiolojia na Vinasaba na maabara ya Mitambo.
-
Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii, Mhe. Aloyce John Kamamba, akizungumza na Wajumbe wa Kamati, Wajumbe wa Bodi pamoja na Watumishi wa Mamlaka (hawapo pichani), baada ya kutembelea Maabara za Mamlaka Februari 4, 2023, kuona namna utekelezaji wa shughuli za uchunguzi unavyofanyika. Mhe. Aloyce amewapongeza Viongozi na Watumishi wa GCLA, kwa kazi kubwa wanayoifanya katika kutekeleza majukumu yao.
-
Jaji wa Mahakama Kuu, Divisheni ya Kazi, Mhe. Biswalo Mganga (kushoto) akiongea na kushauri masuala mbalimbali kuhusu Haki Jinai wakati alipotembelea banda la Mamlaka kwenye Maonesho ya Maadhimisho ya Wiki ya Sheria, yaliyofanyika katika viwanja vya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Kanda ya Dar es Salaam
-
Afisa Sheria kutoka Mamlaka, Eunice Latia (Kulia) akiongea na mmoja wa wadau wa Maonesho ya Wiki ya Sheria aliyetembelea banda la Mamlaka kupata elimu kuhusu Sheria ya Kemikali za Viwandani na Majumbani, kwenye maadhimisho ya Wiki ya Sheria yanayofanyika katika viwanja vya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Kanda ya Dar es Salaam
-
Kamishna Jenerali wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA), Gerald kusaya (kushoto) na Mkurugenzi wa Huduma za Sayansi Jinai, David Elias (kulia) wakiangalia uchunguzi wa awali wa dawa za kulevya unavyofanyika mbele ya waandishi wa Habari na washiriki wengine wa jukwaa la haki jinai (hawapo pichani) ambao ulifanywa na Wakemia, Aston Nathan (katikati) kutoka Mamlaka ya Maabara ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali na Katani Katani (wa pili kulia) kutoka (DCEA) baada ya Kamishna Jenerali, Kusaya, kutembelea maonesho ya maadhimisho ya Wiki ya Sheria yanayofanyika katika Uwanja wa Nyerere Square Jijini Dodoma, Januari 25, 2023.
-
Mkurugenzi wa Huduma za Sayansi Jinai, David Elias (kulia) akiongea na mmoja wa wadau wa maonesho alipotembelea banda la Mamlaka katika maonesho ya maadhimisho ya Wiki ya Sheria yaliyoanza Januari 22, 2023 katika Uwanja wa Nyerere Square Jijini Dodoma.
-
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Philip Mpango (aliyevaa miwani) akiwa pamoja na Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Profesa Ibrahim Juma (wa pili kulia), wakiwa katika matembezi ya ufunguzi wa Maadhimisho ya Wiki ya Sheria yanayofanyika katika Uwanja wa Nyerere Square Jijini Dodoma kuanzia Januari 22 - 29, 2023.
-
Mkemia Mkuu wa Serikali, Dkt. Fidelice Mafumiko (kulia) akimkabidhi nyaraka za Ofisi ya Kanda ya Kaskazini, Meneja mpya wa Kanda hiyo, Eliamini Mkenga (kushoto) ikiwa ni ishara ya kupokea rasmi majukumu ya ofisi hiyo januari 18, 2023.
-
Mtumishi wa Mamlaka aliyekuwa anakaimu Ofisi ya Kanda ya Kaskazini, Erasto Laurence (aliyesimama) akiwasilisha kwa Mkemia Mkuu wa Serikali (aliyekaa katikati) taarifa fupi ya kipindi alichokaimu wakati wa kikao cha kumkabidhi Ofisi Meneja mpya
-
Meneja wa Ofisi ya Kanda ya Kaskazini, Eliamini Mkenga (aliyesimama) akiongea baada ya kukabidhiwa rasmi Ofisi ya Kanda na Mkemia Mkuu wa Serikali, Dkt. Fidelice Mafumiko, Januari 18, 2023 jijini Arusha.
-
Mkemia Mkuu wa Serikali, Dkt. Fidelice Mafumiko (aliyesimama) akiongea na baadhi ya Watumishi wa Ofisi ya Kanda ya kaskazini wakati akimtambulisha na kumkabidhi ofisi hiyo Meneja mpya, Eliamini Mkenga (kushoto) katika tukio lililofanyika Januari 18, 2023 katika ofisi za Kanda zilizopo Sekei jijini Arusha. Kulia ni Mtumishi wa Mamlaka, Erasto Laurence, ambaye alikuwa anakaimu nafasi ya Meneja wa Kanda hiyo baada ya kustaafu Christopher Anyango, Novemba, 2022.
-
Afisa Ustawi wa Jamii, Susan Mdesa (aliyesimama), akiuliza swali na kutaka ufafanuzi juu ya upimaji wa vinasaba vya binadamu kwa wateja wa masuala ya mirathi.
-
Mwezeshaji kutoka Mamlaka,Everlight Matinga (aliyesimama), akitoa ufafanuzi kuhusu majukumu mbalimbali ya Mamlaka ya Maaara ya Mkemia Mkuu wa Serikali (GCLA) wakati wa semina kwa maafisa ustawi wa jamii wa Mkoa wa Dar es Salaam kuhusu Sheria ya Vinasaba vya Binadamu.
-
Mkemia Mkuu wa Serikali, Dkt. Fidelice Mafumiko (aliyesimama), akizungumza wakati akifungua semina ya kuongeza uelewa wa Sheria ya Vinasaba vya Binadamu kwa Maafisa Ustawii wa Jamii Mkoa wa Dar es Salaam iliyofanyika, Disemba 12, 2022 katika ukumbi wa Hazina, jijini Dar es Salaam. Dkt. Mafumiko, amewataka maafisa hao kuendelea kufanya kazi bega kwa bega na Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali huku wakiwa na uelewa wa Sheria ya Vinasaba vya Binadamu Namba 8 ya mwaka 2009 (The Human DNA Act Regulations No.8 of 2009), kwa weledi mkubwa.
-
Washiriki wa mafunzo kutoka Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali (GCLA), wakifuatilia mafunzo ya utekelezaji wa uhakiki wa njia za uchunguzi (Method Validation and Uncertainity of Measurements).
-
Mwezeshaji wa mafunzo, Kezia Mbwambo (aliyesimama), akitoa ufafanuzi kuhusu matakwa ya utekelezaji wa uhakiki wa njia za uchunguzi (Method Validation and Uncertainity of Measurements).
-
Mkemia Mkuu wa Serikali, Dkt. Fidelice Mafumiko (aliyesimama), akifurahia jambo wakati akifungua mafunzo ya utekelezaji wa uhakiki wa njia za uchunguzi (Method Validation and Uncertainity of Measurements), katika ukumbi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Dar es Salaam, 13 Disemba, 2022.
-
Balozi wa Tanzania katika Jamhuri ya Korea ya Kusini, Balozi Togolani Mavura (katikati), Mkemia Mkuu wa Serikali, Dkt. Fidelice Mafumiko (wa tatu kushoto) wakiwa katika Ubalozi wa Tanzania nchini Korea Kusini pamoja na ujumbe alioambatana nao Mkemia Mkuu wa Serikali katika ziara ya mafunzo nchini humo.
-
Mkemia Mkuu wa Serikali, Dkt. Fidelice Mafumiko (wa tatu kushoto) na ujumbe alioambatana nao wakimsikiliza Mwambata wa Ubalozi anayeshughulikia Siasa katika Ubalozi wa Tanzania nchini Korea Kusini, Byakanawa (wa pili kulia) akiwaeleza masuala mbalimbali yakidiplomasia na kiuchumi yanayotekelezwa na ubalozi huo katika nchi ya Korea ya Kusini kwa niaba ya Serikali ya Tanzania.