CHIEF GOVERNMENT CHEMIST

Welcome to the Government Chemist Laboratory Authority (GCLA),your number one centre for laboratory analysis of samples/exhibits related to Forensic Sciences in order to facilitate forensic investigations and hence assurance of justice and rule of law,Read More>>

WORKING HOURS

OFFICES ARE OPEN FROM 8:00 A.M TO 4:00 PM

MONDAY TO FRIDAY EXCEPT PUBLIC HOLIDAYS

 

SOCIAL MEDIA

Twitter icon
Facebook icon
Instagram icon
  • Mwezeshaji wa Mafunzo, Murtaza Versi (kulia) akiwasilisha mada kuhusu “Organizational Culture” kwa Wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka na Sekretarieti yake yaliyofanyika Mei 18, 2023 katika Ofisi za Mamlaka, Makao Makuu, Dodoma.

  • Mwezeshaji wa mafunzo kutoka Ofisi ya Msajili wa Hazina, Hussein Kakurwa (kulia) akiwasilisha mada kuhusu majukumu na wajibu wa Bodi wakati wa mafunzo kwa Wajumbe wa Bodi yaliyofanyika Mei 18, 2023, Dodoma

  • Wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali kutoka kushoto, Zubeda Salum, Dkt. Robert Malima, Dkt. Grace Kinunda na Dkt. Edda Vuhahula, wakiwa kwenye mafunzo kuhusu “organizational Culture” na mafunzo kuhusu usimamizi wa bajeti yaliyotolewa na Ofisi ya Msajili wa Hazina na Murtaza Versi katika ofisi za Mamlaka, Makao Makuu, Dodoma Mei 18, 2023.

  • Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Mamlaka, Profesa Esther Lugwisha (kushoto) na Mkemia Mkuu wa Serikali, Dkt. Fidelice Mafumiko (kulia), wakifuatilia mafunzo kuhusu “organization Culture” yaliyotolewa na Murtaza Versi (hayupo pichani) kwa Wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali yaliyofanyika Makao Makuu ya Mamlaka, Dodoma, Mei 18, 2023.

  • Watumishi wa Mamlaka, wakiwa kwenye uwanja wa Jamhuri mkoani Morogoro mara baada ya kukamilika kwa sherehe za maadhimisho ya Mei Mosi kwa mwaka 2023.

  • Watumishi wa Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali (GCLA), wakiandamana kuelekea katika uwanja wa Jamhuri mkoani Morogoro ambapo Sherehe za maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi duniani zilifanyika kitaifa.

  • Watumishi wa Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali, Ofisi ndogo ya Dar es Salaam na Kanda ya Mashariki, wakiwa katika maandamo ya  Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani (Mei Mosi) kwa Mkoa wa Dar es Salaam, ambapo yamefanyika katika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam Mei 1, 2023.

  • Mkurugenzi wa Uchunguzi wa Bidhaa na Mazingira, Sabanitho Mtega (aliyekaa katikati) na Mkurugenzi wa Huduma za Sayansi Jinai, David Elias (aliyekaa kushoto), wakiwa pamoja na baadhi ya Watumishi wa Mamlaka, Ofisi ndogo ya Dar es Salaam na Kanda ya Mashariki kabla ya kuelekea kwenye Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani 2023 (Mei Mosi) ambapo kwa Mkoa wa Dar es Salaam yamefanyika kwenye Uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam.

  • Watumishi wa Mamlaka, Makao Makuu na Ofisi ya Kanda ya Kati, wakiwa kwenye maandamano ya Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani (Mei Mosi) kwa Mkoa wa Dodoma yaliyofanyika kwenye Uwanja wa Jamhuri Mei 1, 2023.

  • Meneja wa Ofisi ya Kanda ya Kati, Gerald Meliyo (aliyevaa miwani), akiwa pamoja na baadhi ya Watumishi wa Mamlaka, Makao Makuu, Dodoma na Ofisi ya Kanda ya Kati kabla ya kuelekea kwenye Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi 2023 (Mei Mosi) ambapo kwa Mkoa wa Dodoma yalifanyika kwenye Uwanja wa Jamhuri, Dodoma Mei 1, 2023.

  • Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka, Profesa Esther Lugwisha (kulia), Mkemia Mkuu wa Serikali, Dkt. Fidelice Mafumiko (wa pili kulia), Meneja wa Ofisi ya Kanda ya Kusini, Hadija Mwema (wa tatu kulia) pamoja na Watumishi wa Mamlaka walioambatana nao wakimsikiliza Mkurugenzi wa Kiwanda cha Saruji cha Dangote, Normandy Chan (kushoto) mara baada ya kufika katika kiwanda hicho kilichopo mkoani Mtwara kwa ajili ya ukaguzi wa utekelezaji wa Sheria ya Usimamizi na Udhibiti wa Kemikali Aprili 17, 2023. Wa pili kushoto ni Mkuu wa Idara ya usimamizi na Udhibiti Ubora wa Kiwanda cha Dangote, Simon Kikota.

  • Mkemia Mkuu wa Serikali, Dkt. Fidelice Mafumiko (wa tatu kushoto) akiongea na viongozi wa Kiwanda cha Dangote wakiongozwa na Meneja wa Machimbo ya Mawe, Mohamed Mndeme (kulia) wakati akifanya ukaguzi katika maeneo ya Kiwanda cha Dangote mkoani Mtwara Aprili 17, 2023.

  • Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi, Profesa Esther Lugwisha (aliyekaa katikati), Mkemia Mkuu wa Serikali, Dkt. Fidelice Mafumiko (aliyekaa kushoto), Meneja wa Ofisi ya Kanda ya Kusini, Hadija Mwema (aliyekaa kulia) wakiwa pamoja na Watumishi wa Mamlaka kutoka Makao Makuu na Ofisi ya Kanda ya Kusini mara baada ya kumaliza kikao na Watumishi wa Kanda ya Kusini kilichofanyika mkoani Mtwara Aprili 17, 2023.

  • Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka (aliyesimama) akiongea na Watumishi wa Mamlaka Ofisi ya Kanda ya Kusini (hawapo pichani) wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika Kanda hiyo Aprili 17, 2023.

  • Mkemia Mkuu wa Serikali, Dkt. Fidelice Mafumiko (kushoto) akimpongeza Meneja wa Ofisi ya Kanda ya Kusini, Hadija Mwema (kulia) kwa kuaminiwa na kuteuliwa kuiongoza Kanda hiyo wakati akitambulishwa rasmi kwa watumishi na kukabidhiwa Ofisi ya Kanda ya Kusini Aprili 17, 2023.

  • Mkemia Mkuu wa Serikali, Dkt. Fidelice Mafumiko (kulia), akimkabidhi vitendea kazi  Mwenyekiti wa Kamati ya Kitaalam ya Kituo cha Taifa cha Kudhibiti Matukio ya Sumu, Profesa Amos Mwakigonja (kushoto) mara baada ya kuizindua rasmi kamati hiyo Aprili 5, 2023.

  • Mkemia Mkuu wa Serikali, Dkt. Fidelice Mafumiko (aliyekaa katikati), akiwa na Mwenyekiti wa Kamati ya Kitaalam ya Kituo cha Taifa cha Kudhibiti Matukio ya Sumu, Profesa Amos Mwakigonja (aliyekaa kushoto) Katibu wa Kamati, David Elias (aliyekaa kulia) pamoja na Wajumbe wa Kamati (waliosimama) baada ya uzinduzi wa Kamati Aprili 5,2023 jijini Dar es Salaam.

  • Mwenyekiti wa Kamati ya Kitaalam ya Kudhibiti Matukio ya Sumu, Profesa Amos Mwakigonja (wa pili kushoto), akimuuliza swali Meneja wa Maabara ya Maikrobaiolojia, Faustine Wanjala (kulia), kuhusu namna ya uchunguzi wa sampuli mbalimbali unavyofanyika katika maabara hiyo wakati wa kamati hiyo ilipotembelea maabara za Mamlaka Aprili 5,2023.

  • Wajumbe wa Kamati ya Kitaalam ya NPCC wakifuatilia taarifa kuhusu majukumu ya Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali (GCLA) ikiwemo mada kuu kuhusu Uanzishwaji wa Kituo cha Taifa cha Kudhibiti Matukio ya Sumu (NPCC), iliyowasilishwa na Dkt. Fidelice Mafumiko (hayupo pichani).

  • Mkemia Mkuu wa Serikali, Dkt. Fidelice Mafumiko (aliyesimama), akizungumza na Wajumbe wa Kamati ya Kitaalam ya Kituo cha Taifa cha Kudhibiti Matukio ya Sumu (hawapo pichani), wakati akizindua kamati hiyo katika ukumbi wa Mamlaka jijini Dar es Salaam, Aprili 5, 2023. Kushoto ni Mwenyekiti wa Kamati ya Kitaalam ya Kudhibiti Matukio ya Sumu, Profesa Amos Mwakigonja na kulia ni Katibu wa Kamati na Mkurugenzi wa Huduma za Sayansi Jinai wa Mamlaka, David Elias.

  • Mkemia Mkuu wa Serikali Zanzibar, Dkt. Farid Mpatani (kushoto), akiuliza swali kwa Mtaalam wa Maabara, Everlight Matinga (katikati) kuhusu uchunguzi wa maikrobaiolojia mara baada ya kutembelea maabara  ya Maikrobaiolojia wakati wa ziara ya kikazi ya kubadilishana uzoefu na kuimarisha uhusiano wa kiutendaji waliyofanya Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali, Dar es Salaam

  •  Mkemia Mkuu wa Serikali ya Zanzibar, Dkt. Farid Mpatani, (kulia), akimsikiliza Meneja wa Maabara ya Sayansi Jinai Kemia, Fidelis Segumba (kushoto) kuhusu namna uchunguzi wa kimaabara wa dawa za kulevya unavyofanyika katika maabara hiyo wakati wa ziara yake ya kikazi aliyofanya Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali Bara. 

  • Mkemia Mkuu wa Serikali Zanzibar, Dkt. Farid Mpatani (kushoto), akipata ufafanuzi kuhusu uchunguzi wa sampuli mbalimbali za mazingira unavyofanyika kwenye Maabara ya Mazingira kutoka kwa Mtaalam wa Maabara, Alois Ngonyani (kulia) wakati wa ziara ya kikazi aliyofanya Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali Bara.

  • Mkemia Mkuu wa Serikali Zanzibar, Dkt. Farid Mpatani (kushoto), akipata ufafanuzi kuhusu uchunguzi wa sampuli mbalimbali za mazingira unavyofanyika kwenye Maabara ya Mazingira kutoka kwa Mtaalam wa Maabara, Alois Ngonyani (kulia) wakati wa ziara ya kikazi aliyofanya Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali Bara.

  • Watumishi wa Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali, Dar es Salaam, wakiwa pamoja kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja katika kilele cha maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani kwa mwaka 2023.

  • Watumishi wa Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali, Dar es Salaam, wakiandamana na kupita mbele ya mgeni rasmi, Mhe. Amos Makala (hayupo pichani) wakati wa maadhimisho ya siku ya Wanawake Duniani Machi 8,2023, ambapo kwa Mkoa wa Dar es Salaam yalifanyika kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja.

  • Watumishi wa Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali, Dar es Salaam, wakiwa pamoja kabla ya kuelekea viwanja vya Mnazi Mmoja katika kilele cha maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani kwa mwaka 2023.

  • Washiriki wa mafunzo wakimsikiliza Mkemia Mkuu wa Serikali, Dkt. Fidelice Mafumiko (hayupo pichani) akiongea wakati wa kufunga mafunzo ya udhibiti wa Matukio ya sumu kwa Maafisa Afya ya Jamii ngazi ya Kata na Mitaa kutoka Wilaya ya Ilala.

  • Mkemia Mkuu wa Serikali, Dkt. Fidelice Mafumiko (aliyesimama) akiongea wakati wa kufunga mafunzo ya uelewa kuhusu kudhibiti matukio ya sumu kwa Maafisa Afya wa Kata na Wahudumu wa Afya ya Jamii ngazi ya Mitaa. Mafunzo hayo yalifanyika katika makundi mawili, Kundi la kwanza Februari 20, 2023, na kundi la pili Februari 21, 2023 katika Ukumbi wa Tume ya Ushindani, Jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mwakilishi Ofisi ya Mganga Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Anence Kamasho, na kushoto ni Mratibu wa Kituo cha Taifa cha Kudhibiti Matukio ya Sumu, Yohana Goshashy.

  • Mkemia Mkuu wa Serikali, Dkt. Fidelice Mafumiko (aliyesimama), akizungumza na watumishi wa Mamlaka (hawapo pichani), wakati akifungua mafunzo kuhusu Mkakati wa Mapambano dhidi ya Rushwa Mahala pa Kazi. Mafunzo hayo yamefanyika katika ofisi ndogo ya Mamlaka, jijini Dar es Salaam, Februari 17, 2023.

  • Katibu Msaidizi Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma, Dar es Salaam, Bi. Elizabeth Komba (aliyesimama), akiwasilisha mada kuhusu Mkakati wa Mapambano dhidi ya Rushwa Mahala pa Kazi kwa watumishi wa Mamlaka na kuwasisitiza watumishi kuhakikisha wanakuwa waadilifu katika kusimamia shughuli za Serikali.

  • Mkemia Mkuu wa Serikali, Dkt. Fidelice Mafumiko (aliyesimama), akiongea na wanafunzi wa kozi ya Kemia ya Petroli (Petroleum Chemistry), kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, kuhusu majukumu ya Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali (GCLA) katika ukumbi wa Mamlaka uliopo Ofisi ndogo ya Dar es Salaam, Februari 17, 2023. Lengo kuu ya ziara hiyo ni kufahamu namna GCLA, inavyotekeleza majukumu yake mbalimbali haswa katika shughuli za uchunguzi wa kimaabara. Jumla ya Wanafunzi 18 wamepata fursa ya kutembelea Maabara mbalimbali za Mamlaka.

  • Mkurugenzi wa Huduma za Sayansi Jinai, David Elias (aliyekaa katikati), akiwa na Watumishi wa Mamlaka, Meneja wa Maabara ya Maikrobaiolojia, Faustine Wanjala (wa pili kushoto, waliokaa), Kaimu Meneja wa Maabara ya Mazingira, Alois Ngonyani (aliyekaa kushoto) pamoja na wanafunzi wa kozi ya Kemia ya Petroli kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam waliotembelea maabara za Mamlaka kwa ajili ya kujifunza kwa vitendo.

  • Mtumishi wa Mamlaka, Alois Ngonyani (kulia), akiwaelezea wanafunzi wa kozi ya Kemia ya Petroli kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam namna uchunguzi unavyofanyika katika Maabara ya Mazingira.

  • Mtumishi wa Mamlaka, Glory Mushi (kulia), akiwaonyesha kwa vitendo wanafunzi namna uchunguzi wa kimaabara unavyofanyika katika mitando iliyopo katika Maabara ya Mazingira katika Ofisi ndogo ya Dar es Salaam

  • Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Pugu, wakisikiliza mada mbalimbali zilizokuwa zinawasilishwa na maafisa kutoka Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali (hawapo pichani), wakati walipotembelewa na GCLA, kwa lengo la kuwaelimisha kuhusu ya majukumu ya Mamlaka pamoja na matumizi salama ya kemikali.

  • Mtumishi wa Mamlaka, Everlight Matinga (aliyesimama kushoto), akitoa elimu kwa wanafunzi wa Shule ya Sekondari Pugu iliyopo jijini Dar es Salaam, kuhusu majukumu mbalimbali yanayotolewa na Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali (GCLA), yakiwemo Usimamizi wa Sheria ambazo lengo kuu ikiwa ni kulinda usalama wa watu na mazingira katika matumizi ya kemikali na Vinasaba vya Binadamu. Utoaji elimu hiyo umefanyika katika ukumbi wa Shule ya SekondarI Pugu, Februari 17, 2023.

  • Waziri wa Afya, Mhe. Ummy Mwalimu (aliyekaa katikati) Mwakilishi wa Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Daud Masasi (kulia kwa Waziri) Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka, Profesa Esther Lugwisha (kushoto kwa Waziri), Mkemia Mkuu wa Serikali, Dkt. Fidelice Mafumiko(kulia) pamoja na Mkurugenzi wa Tiba kutoka Wizara ya Afya, Profesa Paschal Ruggajo (kushoto) wakiwa pamoja na Wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka na Wakurugenzi wa Wizara ya Afya mara baada ya kukamilika kwa hafla ya kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa Jengo la Makao Makuu ya Mamlaka, jijini Dodoma iliyofanyika Februari 11, 2023

  • Waziri wa Afya, Mhe. Ummy Mwalimu (kulia) na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka, Profesa Esther Lugwisha (kushoto) wakifungua pazia kuashirikia uwekaji rasmi wa jiwe la msingi la jengo la Makao Makuu ya Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali jijini Dodoma Februari 11, 2023.

  • Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka, Profesa Esther Lugwisha, akiongea wakati wa hafla ya kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa jengo la Makao Makuu ya Mamlaka iliyofanyika Februari 11, 2023 katika Ofisi za Mamlaka jijini Dodoma.

  • Waziri wa Afya, Mhe. Ummy Mwalimu (kulia) akitoa hotuba wakati wa hafla ya kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa jengo la Makao Makuu ya Mamlaka iliyofanyika Februari 11, 2023 katika Ofisi za Mamlaka zilizopo Barbara ya Mkemia Mkuu wa Serikali, Mtaa wa Secherela, Kata ya Tambukareli, Kitalu “AC” jijini Dodoma.

  • Mkemia Mkuu wa Serikali, Dkt. Fidelice Mafumiko (kulia) akimkabidhi nyaraka za Ofisi ya Kanda ya Kaskazini, Meneja mpya wa Kanda hiyo, Eliamini Mkenga (kushoto) ikiwa ni ishara ya kupokea rasmi majukumu ya ofisi hiyo januari 18, 2023.

Welcome to the Government Chemist Laboratory Authority (GCLA),your number one centre for laboratory analysis of samples/exhibits related to Forensic Sciences in order to facilitate forensic investigations and hence assurance of justice and rule of law, samples related to agricultural and industrial produce to ascertain safety and quality, samples related to paternity or sex identification in order to address society concerns and samples related to environmental and occupational health for the protection of health and the environment.Read More>>


Error message

Notice: Undefined offset: 1 in counter_get_browser() (line 71 of /var/www/gclawebsite/sites/all/modules/counter/counter.lib.inc).

Mission Vision and Core Values

  • Vision

 

To become a reputable world class analytical laboratory for executing health, social well-being and environmental interventions.

 

 

 

  • Mission

 

To provide quality and cost effective laboratory and regulatory services to the Government, Institutions, private sector and the general public for the purpose of safeguarding human health, environment and for execution of justice

 

 

  • Core Values

 

In pursuit of provision of quality services we shall be guided by the seven core values, which are: Quality Service Delivery , Professionalism , Accountability , Team Spirit,

Diversity , Transparency,Loyalty to Government, Integrity



Copyright ©2023 Government Chemist Laboratory Authority. All Rights Reserved.

Designed and Mantained by GCLA ICT Team.