Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro, Murtallah Sadiki (kushoto) akisaini kitabu cha wageni mbele ya Mtumishi wa Mamlaka, Sadock Mboya (kulia) wakati alipotembelea banda la Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali kwenye maonesho ya wiki ya Sheria katika viwanja vya Nyerere Square jijini Dodoma.
Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Mtwara, Abeid Kafunda (kushoto) akisaini kitabu cha wageni mbele ya Mtumishi wa Mamlaka, Sadock Mboya (kulia) wakati alipotembelea banda la Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali kwenye maonesho ya wiki ya Sheria katika viwanja vya Nyerere Square jijini Dodoma.
Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Mjini, Jabir Shekimweri (kulia) akisikiliza maelezo kutoka kwa mtumishi wa Mamlaka, Sadock Mboya (kushoto) juu ya majukumu la Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali kwenye mnyororo wa Haki jinai, wakati alipotembelea banda la Mamlaka kwenye maonesho ya wiki ya Sheria katika viwanja vya Nyerere Square jijini Dodoma.
Msajili Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. Eva Kiaki Nkya (kulia) akimkabidhi cheti cha ushiriki Mkurugenzi wa Huduma za Sayansi Jinai wa Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali, David Elias (kushoto) wakati akifunga maonesho ya wiki ya Sheria katika viwanja vya Nyerere Square jijini Dodoma Februari 1, 2025. Katikati ni Msajili wa Mahakama ya Rufani, George Herbert.
Msajili Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. Eva Kiaki Nkya, akiongea wakati wa kufunga maonesho ya wiki ya Sheria katika viwanja vya Nyerere Square jijini Dodoma Februari 1, 2025.
Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Prof. Elisante Olle Gabriel (kushoto) akimsikiliza Mkurugenzi wa Huduma za Sayansi Jinai wa Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali, David Elias (kulia) wakati alipotembelea banda la Mamlaka katika maonesho ya wiki ya Sheria yanayofanyika katika viwanja vya Nyerere Square jijini Dodoma Januari 27, 2025.
Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Prof. Elisante Ole Gabriel (wa pili kushoto) akitoa pongezi kwa GCLA kwa utoaji huduma bora za uchunguzi wa kimaabara wa sampuli za jinai wakati alipotembelea banda la Mamlaka katika maonesho ya wiki ya Sheria yanayofanyika katika viwanja vya Nyerere Square jijini Dodoma, Januari 27, 2025.
Meneja wa Mamlaka, Ofisi ya Kanda ya Kusini, Hadija Mwema (katikati) akiwa na watumishi wa Mamlaka pamoja na washiriki wa Mafunzo ya Usafirishaji Salama wa Kemikali yaliyofanyika kwa siku mbili katika ukumbi wa Heritage Cottage – Msamala, mjini Songea, Ruvuma.
Washiriki wa Mafunzo ya Usafirishaji Salama wa Kemikali wakifuatilia mada mbalimbali zilizowasilishwa na wataalam kutoka Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali kutoka Ofisi ya Kanda ya Kusini.
Meneja wa Mamlaka Ofisi ya Kanda ya Kusini, Hadija Mwema, akifungua mafunzo ya usafirishaji salama wa kemikali kwa madereva wanaosafirisha mizigo hatarishi yaliyofanyika katika ukumbi wa Heritage Cottage, Songea, Ruvuma Desemba 17 hadi 18, 2024.