Mtumishi wa Mamlaka, Onesphat Stephano (kushoto) akitoa elimu juu ya majukumu ya Mamlaka kwa wananchi waliotembelea banda la Mamlaka katika maonesho ya Wiki ya Afya na Usalama kazini yanayofanyika katika viwanja vya General tyre jijini Arusha.
Mtumishi wa Mamlaka, Selina Maghembe (kulia) akitoa elimu juu ya majukumu ya Mamlaka kwa mtumishi wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) alipotembelea banda la Mamlaka katika maonesho ya Wiki ya Afya na Usalama kazini yanayofanyika katika viwanja vya General tyre jijini Arusha Aprili 27, 2024.
Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya Wakala wa Afya na Usalama Mahali pa Kazi (OSHA), Dkt. Adelhelm Meru (kushoto) akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kutembelea banda la Mamlaka kwenye maonesho ya Wiki ya Afya na Usalama Kazini yanayofanyika katika viwanja vya General tyre jijini Arusha Aprili 27, 2024. Kulia ni Meneja wa Ofisi ya Kanda ya Kaskazini, Eliamini Mkenga.
Mkemia Mkuu wa Serikali, Dkt. Fidelice Mafumiko na Meneja wa Ofisi ya Kanda ya Kati, Gerald Meliyo (kulia) wakimsikiliza Meneja Ubora wa Kiwanda cha kuchakata Pareto, Paul Looken (kushoto) akieleza namna wanavyofanya uchunguzi wa kimaabara kujua ubora wa mazao ya pareto wanayonunua kutoka kwa wakulima wakati wa ukaguzi wa maabara ya kiwanda hicho kilichopo Mafinga wilayani Mufindi uliofanyika kiwandani hapo Aprili 17, 2024.
Mkemia Mkuu wa Serikali, Dkt. Fidelice Mafumiko (kulia) na Meneja wa Ofisi ya Kanda ya Kati, Gerald Meliyo na Mkaguzi wa Kemikali, Revocatus Mwamba (kushoto) wakikagua stoo ya kemikali katika Kiwanda cha Lush Chanzo na kutoa maelekezo ya kufanyia kazi mapungufu waliyoyaona katika kiwanda hicho wakati wa ukaguzi uliofanyika Aprili 17, 2024.
Mkemia Mkuu wa Serikali, Dkt. Fidelice Mafumiko (kushoto), akitoa maelekezo kwa Msimamizi wa Kiwanda cha Lush Chanzo, kufanyia kazi mapungufu yaliyoonekana upande wa chini wa matanki yanayotumika kuchanganya kemikali kwa ajili ya kutengeneza gundi inayotumika kutengenezea mbao za kutengeneza samani katika kiwanda hicho wakati wa ukaguzi uliofanyika Mafinga Aprili 17, 2024.
Mkemia Mkuu wa Serikali, Dkt. Fidelice Mafumiko (kushoto), akitoa maelekezo kwa Msimamizi wa Kiwanda cha Lush Chanzo, kufanyia kazi mapungufu yaliyoonekana upande wa chini wa matanki yanayotumika kuchanganya kemikali kwa ajili ya kutengeneza gundi inayotumika kutengenezea mbao za kutengeneza samani katika kiwanda hicho wakati wa ukaguzi uliofanyika Mafinga Aprili 17, 2024.
Mkemia Mkuu wa Serikali, Dkt. Fidelice Mafumiko (kushoto) na Meneja wa Ofisi ya Kanda ya Kati, Gerald Meliyo (kulia) wakitoa maelekezo kwa Msimamizi wa Kiwanda cha Lush Chanzo, kufanyia kazi mapungufu yote waliyoyaona katika eneo la kuchanganya kemikali katika kiwanda hicho wakati wa ukaguzi uliofanyika Aprili 17, 2024.
Mkemia Mkuu wa Serikali, Dkt. Fidelice Mafumiko (wa pili kulia) akikagua nyaraka zilizobandikwa eneo la kuchanganyia kemikali zikieleza mambo ya msingi ya kuzingatia wakati wa kutumia kemikali katika kiwanda cha Lush Chanzo, wakati wa ukaguzi katika kiwanda hicho kilichopo eneo la Kinyanambo, Wilaya ya Mufindi mkoani Iringa, Aprili 17, 2024. Kulia ni Meneja wa Ofisi ya Kanda ya Kati, Gerald Meliyo.
Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Nguvu za Atomu Tanzania (TAEC), Prof. Lazaro Busagala (wa tano kutoka kushoto) aliwa pamoja na timu ya washiriki pamoja na kamati ya maandalizi wa zoezi la utayari dhidi ya dharura za kikemikali na kimionzi Tanzania (ZOKIKITA 2024) baada ya kuzinduliwa zoezi hilo na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, jijini Dar es Salaam.